<sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
<noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>

    久久精品蜜芽国产亚洲av,国产成人观看免费全部完,1024综综合合久久AV,午夜国产成人精品,国产精品综合承认,国产高跟黑色丝袜在线

    Mji wa Beijing, China wavunja rekodi za utalii wakati wa likizo ya "wiki ya dhahabu"

    (Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 08, 2024

    Watalii wakijipiga picha za selfie kwenye Bustani ya Tiantan mjini Beijing (Hekalu la Mbinguni/ Temple of Heaven)  Oktoba 1, 2024. (Picha na Chen Xiaogen/Xinhua)

    Watalii wakijipiga picha za selfie kwenye Bustani ya Tiantan mjini Beijing (Hekalu la Mbinguni/Temple of Heaven) Oktoba 1, 2024. (Picha na Chen Xiaogen/Xinhua)

    BEIJING - Wakati wa likizo ya "wiki ya dhahabu" ambayo ni likizo ya Siku ya Taifa ya China iliyoanza Tarehe Mosi, Oktoba hadi jana Jumatatu Oktoba 7, mji wa Beijing ambao ni mji mkuu wa China umeweka rekodi mpya za idadi kubwa ya watalii na mapato ya jumla yatokanayo na shughuli za utalii.

    Takwimu za Idara ya Utamaduni na Utalii ya Mji wa Beijing zinaonyesha kuwa wakati wa likizo hiyo, mji mkuu huo wa China ulipokea watalii milioni 21.6, ikifikia ongezeko la 18.35% kuliko lile la likizo kama hilo la mwaka uliopita. Wakati huo huo, mji huo umepata mapato ya jumla ya shughuli za utalii ya yuan bilioni 26.9 (sawa na dola za Kimarekani bilioni 3.8), imeongezeka kwa asilimia 11.67 ikilinganishwa na mwaka uliopita.

    Ukiwa ni kituo cha utamaduni cha kuvutia chenye mabaki ya alama ya historia kama vile Forbidden City na Ukuta Mkuu, ambapo mambo ya jadi za kale na maendeleo ya kisasa yanayofungamana yameufanya mji huo kuwa mji wenye vivutio kwa watalii wanaotaka kuchangamana katika utamaduni wa China.

    Eneo la mstari wa katikati wa Beijing lililotambuliwa na UNESCO kuwa ni Mali ya Urithi ya Dunia yenye urefu wa kilomita 7.8 limewapa watalii namna mpya ya kutalii mji huo kupitia kutembea kwa miguu. Shauku ya watalii kutembelea kwenye kando za mstari wa katikati wa mji imeongezeka kwa kiasi kikubwa, huku oda zikiongezeka kwa asilimia 69 ikilinganishwa na mwaka jana.

    Kadiri mkakati wa ustawishaji wa vijiji wa China unavyoendelea siku hadi siku, ndivyo miundombinu bora, huduma bora na shughuli mbalimbali za kuvutia zinavyovutia zaidi watalii kufanya safari za muda mfupi kwenye maeneo ya vijijini katika miaka ya hivi karibuni.

    Katika kipindi cha likizo hiyo, maeneo ya vijijini ya Beijing yalipokea watalii jumla ya milioni 4.5, na kupata ongezeko la asilimia 13.6 kuliko kipindi kama hicho cha mwaka uliopita, huku mapato yatokanayo na uendeshaji yakifikia yuan milioni 602, ikiwa ni ongezeko la asilimia 4.5 kuliko lile la kipindi kama hicho cha mwaka uliopita.

    Aidha, wakati wa likizo hiyo ya wiki nzima, idara za utamaduni za umma za Beijing ziliandaa shughuli jumla ya 855, zikiwemo maonyesho, mihadhara ya utamaduni, shughuli za kusoma vitabu, mafunzo ya sanaa na kujionea mali za urithi wa utamaduni usioshikika, zikivutia washiriki 446,900.

    Jumla ya maonyesho 2,071 ya kibiashara yalifanyika, ikiwa ni asilimia 14 zaidi ya yale ya kipindi kama hicho mwaka uliopita.?

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

    Picha

    久久精品蜜芽国产亚洲av
    <sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
    <noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>