<sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
<noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>

    久久精品蜜芽国产亚洲av,国产成人观看免费全部完,1024综综合合久久AV,午夜国产成人精品,国产精品综合承认,国产高跟黑色丝袜在线

    Shirika la ndege la Kenya Airways lazindua kampeni ya kuvutia watalii wa China

    (Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 24, 2024

    NAIROBI - Shirika la ndege la Kenya Airways limesema Jumatatu kwamba limeanzisha kampeni ya kuvutia wasafiri zaidi wa China kutembelea nchi hiyo.

    Julius Thairu, afisa mkuu wa biashara na wateja wa shirika hilo la ndege, amesema kampeni hiyo inajikita katika kuongeza uelewa kwa wananchi wa China kuhusu vivutio vya utalii vya Kenya, kama vile mbuga za wanyama.

    "Tunashirikiana na mawakala wa safari za watalii na mashirika ya ndege ya China ili kuongeza watalii wa China wanaoingia nchini Kenya," Thairu amesema kwenye mahojiano na Shirika la Habari la China, Xinhua katika mji mkuu wa Kenya, Nairobi.

    Kwa mujibu wa takwimu za Bodi ya Utalii ya Kenya, ambalo ni shirika la serikali la utangazaji utalii, raia takriban 52,000 wa China walitembelea Kenya mwaka 2023.

    Amebainisha kuwa Kenya Airways kwa sasa hufanya safari mara tano kwa wiki kati ya Nairobi na Guangzhou, mji mkuu wa Mkoa wa Guangdong kusini mwa China.

    Thairu ameongeza kuwa Kenya Airways inajipanga kuongeza idadi yake ya safari za ndege na kuanza safari za kuelekea Beijing ili kutumia kikamilifu fursa ya sekta ya utalii ya China inayokua.

    Shirika la Kenya Airways tayari limeingia makubaliano ya kugawana huduma za kibiashara na mashirika ya ndege ya China Southern na China Eastern.

    (Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

    Picha

    久久精品蜜芽国产亚洲av
    <sup id="ggg8g"><ul id="ggg8g"></ul></sup>
    <noscript id="ggg8g"></noscript>
  • <nav id="ggg8g"><code id="ggg8g"></code></nav>
  • <sup id="ggg8g"><delect id="ggg8g"></delect></sup>
  • <small id="ggg8g"><menu id="ggg8g"></menu></small>